Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania IGP Simon Sirro Afanya Uhamisho wa Makamanda
MKUU wa Jeshi la Polisi (IGP), Simon Sirro amefanya uhamisho na mabadiliko ya baadhi ya Makamanda wa Polisi wa Mikoa ambapo amemuhamisha RPC wa Dodoma Onesmo Lyanga kwenda Makao Makuu ya Polisi Dodoma na nafasi yake imechukuliwa na aliyekuwa RPC Kaskazini Unguja, Martin Otieno.
Aliyekuwa Mkuu wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Kanda Maalum ya Dar es salaam, Daniel Shillah amehamishwa kwenda kuwa RPC Kaskazini Unguja.