The House of Favourite Newspapers

Mkwaju mpya wa Dogo Janja huu hapa

0

Janjaro2_NoizDogo  kutoka Kundi la Tip Top lenye maskani yake Manzese jijini Dar, Abdulaziz Chande, Dogo Janja.

Omary Mdose, Dar es Salaam
DOGO kutoka Kundi la Tip Top lenye maskani yake Manzese jijini Dar, Abdulaziz Chande maarufu kama Dogo Janja, kuanzia kesho Alhamisi ngoma yake mpya inayokwenda kwa jina la My Life inatarajiwa kuanza kusikika katika vituo mbalimbali vya redio hapa nchini.
Dogo Janja ambaye amewahi kutoa ngoma kadhaa zinazoongelea kipaji chake kama Anajua aliyofanya na Tunda Man, safari hii amekuja na wimbo unaozungumzia maisha yake yote aliyopitia mpaka kufikia hapo alipo utakaojulika kama My Life.

becbfde958aa85806ed0dcb390338c3eKiongozi wa Kundi la Tip Top, Hamad Ally ‘Madee’ amefunguka kuwa ndani ya mwaka huu kundi lao limedhamiria kuteka soko la muziki nchini na kila mwezi memba wao mmoja atakuwa akiachia ngoma.
“Malengo ya kundi letu mwaka huu ni kutoa ngoma baada ya ngoma kwa kila msanii, tumepanga kila mwezi msanii mmoja aachie ngoma, mwezi wa kwanza ameanza Tunda Man akatoa Mama Kijacho, mwezi huu ni zamu ya Dogo Janja ambaye ngoma yake inatoka Alhamisi (kesho) itakayokwenda kwa jina la My Life.
“Humo ndani inazungumzia maisha halisi ya Dogo Janja kuanzia alipotoka mpaka alipo sasa ikiwemo pia maisha yake ya kimapenzi,” alisema Madee.

Leave A Reply