Morrison Atwaa Tuzo ya Mchezaji Bora wa Mwezi Juni
KIUNGO Mshambuliaji wa Simba raia wa Ghana, Bernard Morrison, amekabidhiwa kitita cha shilingi Ml 1, kutoka kampuni ya Emirates Alluminium baada ya kutwaa tuzo ya mchezaji bora wa Mwezi Juni, kutoka Simba, huku akiwagaragaza, Luis Miquissone na Nahodha wake John Bocco, ambapo walikuwa wakiwania tuzo hiyo pamoja.
Tuzo hiyo imekuwa ikitolewa na Kampuni ya Emirates Alluminum kila mwezi, huku mchakato wa kumpata mshindi huendeshwa na Simba kupitia kura za mashabiki wa klabu hiyo.