Mpoto Afunguka Sakata la Madawa ya Kulevya
MWANAMUZIKI wa muziki wa asili Bongo, Mrisho Mpoto, amefunguka kuhusu ishu ya madawa ya kulevya kwa kueleza dawa hizo zinavyoathiri nguvu-kazi ya taifa.
Kupitia mtandao wa kijamii, Mpoto ameweka picha ikiwaonyesha vijana wamemzunguka Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, ikienda sambamba na ujumbe huu unaosema kwamba:
“Unga unamaliza nguvu-kazi ya taifa, huu ni muonekano wa vijana wa kesho tukichelewa kushirikiana, ” aliandika Mpoto.
Aidha, Mpoto aliyewahi kuwa balozi wa amani nchini, alisema kwamba amani haipatikani kwenye utegemezi na haiendani na vitendo vya uhalifu. Unga unapoteza nguvu-kazi na kuchochea uhalifu.
Katika ujumbe huo, Mpoto ameomba ushirikiano ili kuwanusuru vijana ambao ndiyo taifa la leo.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam katikati aliyekaa chini amezungukwa na vijana watumiaji wa dawa za kulevya.
Comments are closed.