Mkali wa tungo za Kiswahili aliyejizolea umaarufu mkubwa Bongo kutokana na ujumbe unaobebwa kwenye mashairi yake, Mrisho Mpoto ‘Mjomba’, leo ametembelea ofisi za Global Publishers, Bamaga-Mwenge jijini Dar es Salaam.
Mbali na kujionea jinsi kazi zinazofanyika, Mpoto anayetamba mitaani na wimbo wake wa Sizonje, pia amefanya mahojiano maalum na Global TV Online ambapo amezungumzia mambo mbalimbali kuhusu maisha yake ya kimuziki, mafanikio na changamoto anazokutana nazo.
Mahojiano kamili yatakujia muda mfupi baadaye kwa kupitia Global TV Online.
Comments are closed.