The House of Favourite Newspapers

Msemaji wa Serikali Atoa Pongezi Kwa Wafanyakazi wa Global

Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) ambaye pia ni Msemaji wa Serikali Bw. Hassan Abbas akifika katika Ofisi za Global Group zilizopo Sinza Mori jijini Dar es Salaam, leo.
Mhariri Mtendaji wa Global Publishers, Saleh Ally akisalimiana na Bw. Abass
Wageni walioongozana na Bw. Abass wakisalimiana na wenyeji wao.
…Akisaini kitabu cha wageni.
…Akioneshwa makampuni yaliyopo kwenye Jengo la Global Group.
Mkurugenzi wa Global Group, Eric Shigongo (kushoto) akizungumza na Bw. Abass.
…Akisalimiana na Mhasibu Mkuu wa Global Group, Lawrance Kabende.
…Akibadilishana mawazo.
…Akisalimiana na Mhariri wa Gazeti la Championi Jumatatu, Ezekiel Kitula.

Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) ambaye pia ni Msemaji wa Serikali Bw. Hassan Abbas, leo ametembelea Ofisi za Global Group zilizopo Sinza Mori jijini Dar es Salaam.

Katika ziara yake hiyo, Bw. Abass aliipongeza Global Group kutokana na suala zima la habari kutokana na kuwa na watu wenye weledi wa hali ya juu, huku pia akipongeza namna kampuni hiyo inavyozalisha magazeti.

Bw. Abass amewataka waandishi wa habari kujiendeleza zaidi angalau kufikia levo ya diploma kwa wale ambao hawajafika levo hiyo kutokana na sheria waliyoiweka ambayo hapo baadaye wanahabari wote watatakiwa kuwa na angalau diploma ya uandishi wa habari.

 

 

Comments are closed.