The House of Favourite Newspapers

Mtoto Auawa Shuleni kwa Kunyweshwa Kemikali

0

ZAIDI ya watu 180,000 wametia saini maombi ya kudai haki baada ya kifo cha mwanafunzi Sylvester Oromoni wa shule ya bweni mwenye umri wa miaka 12 nchini Nigeria.

 

Familia ya Oromoni imewashutumu wanafunzi wenzake watano katika Shule ya Dowen huko Lagos kwa kumtesa kwa sababu alikataa kujiunga na kikundi cha madhehebu. Kifo chake kimewakasirisha wengi nchini Nigeria na shule imefungwa kwa muda usiojulikana.

 

Katika taarifa yake, Shule ya Dowen kilisema kijana huyo alifariki kutokana na majeraha aliyoyapata wakati akicheza soka. “Uchunguzi wa awali ulionesha kuwa hakuwa amepigana, kuonewa au aina yoyote ya shambulio dhidi ya mtoto huyo,” ilisema.

 

“Ninachotaka ni haki,” baba yake Sylvester alisemahuku akipinga maelezo ya shule kuhusu kilichotokea. Mwanafamilia mwingine ambaye ni binamu yake Sylvester anaeleza tukio hilo kivingine. Alidai kupitia mtandao wa Twitter kwamba wavulana watano walimkamata Sylvester, wakamfungia katika hosteli yake na kumpa kemikali ya kunywa.

Leave A Reply