The House of Favourite Newspapers

Mtoto wa miaka 14 Aibuka Kinara wa Mashindano ya Kuhifadhi Qur-an

0
Khamis Said ameibuka kinara kuhifadhi Qur- an kwa juzuu kumi katika mashindano madogo yaliofanyika leo akisikiliza jambo
Baadhi ya Washiriki wakifuatilia jinsi wenzao wanavyosoma Quran kwenye mashindano hayo.

KIJANA wa miaka 14, Khamis Said ameibuka kinara kuhifadhi Qur- an kwa juzuu kumi katika mashindano madogo yaliofanyika leo Jumatatu kwenye msikiti wa Al Fattah, Keko Jijini huku mgeni rasmi akiwa ni alozi wa Iran, Ameer Mohammed Khan.

Katika mashindano hayo yalioshirikisha washiriki katika makundi sita ambapo ni kundi la juzuu moja, tatu, tano, kumi, 15 na  20 ambapo kijana huyo amefanikiwa kushinda na kupewa zawadi ya godoro la nchi 12 na pesa shilingi  160000, mshindi wa pili, Abduulkarim Bakari amepata godoro la nchi kumi na pesa shilingi 155000 huku mshindi wa tatu, Hindu Khamis akipata pia godoro la nchi 8 na pesa shilingi 150000.

Katika kundi la juzuu ya kwanza washindi ni  Mariam Selema amepata zawadi ya dinner set  ya PC 50 na glass,  wapili  Yassir Khamis (Dinner set 47)  na watatu ni Rahma Juma (Hot Pot Pc 4), wengine  katika  kundi la juzuu ya tatu  kwa upande wa wavulana ni Ibrahim Abdurahman (Godoro nchi kumi), Ausi Sadat (Godoro nchi  nane) na Iddrisa Swalihina  (Godoro nchi sita).

Kwa upande wa wasichana kwa juzuu tatu washindi ni Mwajuma Said (Godoro nchi nane), Zuwena  Salum (Godoro nchi  sita),  Aisha Suleman (Dinner Set  Pc 50). Washindi wa juzuu tano ni  Suleiman Omary (Cherehani),  Asma  Mohammed (Godoro nchi 12) na Maliki Said (Godoro nchi nane). Washindi wa Juzuu kumi ni  Asma Swaleh ( Godoro nchi kumi na pesa 140000), Hajra  Twahir (Godoro nchi kumi na pes  130000) na Laila Ismail ( Chereheni na pesa shilingi 70000).

Washindi wa juzuu 15 ni Rehema Issa amepata godoro na pesa shilingi 155000, Ramadhani Iddy  amepewa godoro  na pesa shilingi 150000 na Ibrahim Said zawadi ya godoro na pesa shilingi 45.

 

Breaking News: Mabilionea wa Escrow Wasoteshwa Mahakama ya Kisutu, Wapigishwa Magoti Hadharani

Leave A Reply