The House of Favourite Newspapers

MTOTO WA RAY ALAMBA SHAVU NMB

Ray akizungumza wakati wa utambulisho huo.

 

MTOTO wa Staa wa Filamu Bongo, Vicent Kigosi ‘Ray’, aitwaye Jaden Kigosi, amepata shavu kutoka kwa wazazi wake baada ya kumfungulia  akaunti ya ‘NMB Mtoto Akaunti’ kwa ajili ya akiba itakayoweza kumsaidia hapo baadaye.

Kutoka kushoto ni Ofisa Msimamizi wa bidhaa NMB, Hezbon Mpate, Vicent Kigosi, Chuchu Hans na Meneja Huduma za Kibenki  NMB, Caroline Mosha.

 

Akizungumza na waandishi wa habari  wakati wa kumfungulia akaunti hiyo, Makao Makuu ya Benki ya NMB, Posta jijini Dar, Ray alisema kuwa, huo ni uamuzi aliouchukua yeye na mwenzi wake  Bi Hans baada ya kuridhishwa na huduma za Benki ya hiyo. Pia kutokana na kushawishika na umahiri wa umahususi wa akaunti hizi za mpango wa NMB Mtoto Akaunti.

 

“Niwaombe tu mastaa wenzangu kuwa, suala la mtoto kumfungulia akaunti benki ni muhimu sana kwani sisi wazazi tupo leo lakini hatujui kesho yetu itakuwaje?

Chuchu Hans na mwanaye Jaden.

“Ili usimnyime haki ya maisha mazuri mwanao hapo baadaye, basi ni jukumu la kila mmoja kuhakikisha anamfungulia akaunti mwanaye ila hata asipokuwepo ataweza kusoma bila shida,” alisema Ray.

Ray akisaini mkataba. Kulia anayemsainisha ni Meneja Huduma za Kibenki  NMB, Caroline Mosha.

Ray aliambatana na mzazi mwenzake ambaye pia ni msaniiwa Bongo Movies, Chuchu Hans katika kumfungulia mtoto wao NMB Mtoto Akaunti.

Ray na mwanaye Jaden.

Kwa upande wake Meneja Huduma za Kibenki  NMB, Caroline Mosha, ametoa wito kwa walezi na wazazi kuwa na utamaduni wa kuwafungulia akaunti watoto na vijana wao bila kusahau kuwahimiza kuhusu elimu ya fedha#NMBWajibu. www.nmbbank.co.tz/wajibu

Musa Mateja

 

Comments are closed.