The House of Favourite Newspapers

Mume wa Uwoya Azikwa Nchini Rwanda, Mamia Wajitokeza Kumzika

0
Wachezaji wa timu ya Rayon Sports Ismailla Diarra (kushoto) na Tidiane Kone (kulia),wakiwa wamebeba mwili wa marehemu  Hamadi  Ndikumana Katauti kutoka nyumbani kwake Nyakabanda kwenda katika Msikiti Qaddafi uliopo Nyamirambo, Rwanda na baadaye walifanya mazishi jana jioni.
Baba mzazi wa Ndikumana baada ya kuwasili nyumbani kwa aliyekuwa mwanae, Ndikumana akitokea burundi.
Mama mzazi wa Ndikumana akisadiwa amebebwa baada ya kufika Nyumbani kwa mwanae Rwanda akitokea Burundi.
Majirani wakiwa wanalia.
Watoto wakiwa barabarani kuaga mwili wa Ndikumana wakati ukipelekwa katika Msikiti wa Qaddafi  uliopo Nyamirambo, Rwanda.
…Safari ya Kupeleka mwili wa marehemu msikitini ikiendelea.
Ndugu wa Ndikumana akilia kwa uchungu.
Baadhi ya waombolezaji wakiwa barabarani wakati wa kusindikiza mwili wa marehemu
Majirani wakiwa msibani kwa Ndikumana.
Wakiendelea kuelekea msikitini.

MWILI wa nahodha wa zamani wa timu ya taifa ya Rwanda, Hamadi  Ndikumana Katauti (39)   amezikwa jana kufuatia kufariki  nyumbani kwake usiku wa kuamkia juzi,  nchini Rwanda katika makaburi  yaliokuwepo kwenye mji wa Nyamirambo, Rwanda.

Ndikumana ambaye  alikuwa mume wa muigizaji wa filamu nchini, Irine Owoya amezikwa na mamia ya wadau wa soka nchini humo wakiwemo mashabiki wa klabu ya Rayon  Sport ambayo alikuwa akifanyia kazi kama kocha msaidizi.

Leave A Reply