ZOEZI LA kukinasua Kivuko cha Mv.Nyerere imesimama kwa muda baada ya mnyororo uliokuwa ukitumika kukivuta kukatika, ambapo juhudi za kuunganisha zinaendelea wataalam wa vikosi vya uokoaji, wakiwemo askari wa jeshi la wananchi wa Tanzania.
Zoezi hilo limesimama baada ya asubuhi ya leo kuanza kuonyesha matumaini ya kukinyanyua ambapo sehemu ya mbele ya nahodha na maandishi ya MV. Nyerere kuanza kuonekana.
Comments are closed.