The House of Favourite Newspapers

Mwana FA: Dume Suruali Darasa Kwa Kizazi Cha Digitali

MWANA-FA-12 Msanii wa Bongo Fleva, Mwana FA 

Na John Joseph

WIMBO wa Dume Suruali ndiyo inawezekana ukawa msemo kwa Watanzania wengi kwa kipindi cha miezi kadhaa ijayo, hiyo ni kutokana na mashairi yaliyoandikwa na mtunzi wa wimbo huo, Mwana FA akimshirikisha V-Money.

Unazungumzia mwanaume anavyolalamika kulazimishwa kuhonga fedha kwa mwanamke. Mwan FA ambaye jina lake halisi ni bwana Hamisi Mwinjuma, amezungumza na gazeti hili kufafanua kile alichokiandika kwenye wimbo huo aliomshirikisha bi Vanessa Mdee:

Lengo lako hasa ni nini?

Ni kuwataka watu wasiwe wajinga kwa kuwa mapenzi ni hisia na siyo biashara. Matukio kama hayo yamekuwa yakitokea mara nyingi tu katika kizazi cha sasa. Sina maana ya kuwasema vibaya wanawake lakini tukumbuke hata upande wetu sisi wanaume kuna Malioo ambao wao wanapenda kuhongwa na wanawake, ujumbe huu ni maalum kwa pande zote.

mwana-faKwa nini Vanessa?

Vanessa ni aina ya wanawake ambao sisi wanaume tukimuona tunahisi ili umpate ni lazima umuhonge sana, sababu ya kumchagua yeye ni kwa kuwa anawakilisha vizuri wasichana wa aina hiyo ambao wengi wamekuwa na mitazamo hiyo.

Umetunga kwa kuwa yamekutokea?

Mimi ni msanii, nawakilisha mengi yanayotokea kwenye jamii, yapo yaliyonitokea na mengine watu wangu wa karibu na jamii kwa jumla, kuna vitu ambavyo unaongeza ili sanaa ikamilike lakini kwa ufupi nimezungumza ukweli.

Utunzi wa wimbo ulikuwaje?

Niliutunga ndani ya muda wa siku moja niliyoenda studio lakini ilinichukua mwezi mzima kuwa naurekebisha hapa na pale. Hata Vanessa nilipomweleza alikubaliana na wazo langu na kuamini utafanya vizuri.

Kwa nini ulichagua MJ Records?

Prodyuza wa wimbo huo ni Daxo Chali ambaye ni mdogo wake Marco Chali. Nilienda MJ kwa Marco nikamueleza nataka kazi fulani akanipa ‘beat’ mbili, nikachagua yangu na Vanessa naye akachagua hii ambayo ndiyo imetumika kwenye wimbo.

Tuliamua kuchagua hiyo kwa kuwa Vanessa alinishauri ni beat laini ambayo kwanza itakuwa na ladha tofauti ndiyo maana tukaitumia.

vanessa (2)-001Msanii wa Bongo Fleva, Vanessa ‘V-Money’.

Umemtaja tajiri Salah kwenye wimbo, ni nani?

Huyu ni rafiki yangu wa karibu, ni mmoja wa watu wangu ambaye amekuwa anashangaa sana jinsi wanaume wanavyohonga.

Mashairi ya Dume Suruali

Mwana FA

Hudat hudat hii ni salam na ufahamu

Kama unauza mapenzi siyo kwa binamu

Huna haja ya kusubiri hii ni hukumu

Hakuna kitu utapata utangoja kama askari wa zamu

Dume suruali dume kaptula

Shauri zako ilimradi sipati hasara

Usione utani me sihongi hata kwa ishara

Utaniambia nini mpaka unigeuze fala

Kwanza nasikia hongo zinaleta mkosi

Sentano yangu hugusi hata ukiongea kidosi

Yabaki mapenzi tusileteane ujambazi

Hata upige sarakasi utachonga viazi.

BAHILI KAMA NINI!!!!!!!!! Ndiyo mnavyosema

Na ukiniomba kesho hunisikii tena

Kwani unauza nini dada!

Hunitakii mema.

Kiitikio

We dume suruali kaa mbali nami

Kama dume suruali kaa mbali nami

Huendani na mimi

I want Gucci, Fendi, spend it on the girl like me

My name is Vee Money, money spend on the girl like me

MWANA FA

Nihonge nanunua nini kwa nini yaani!

Kuna kipi nisichokijua ina TV ndani?

Usiulize n’takupa nini dada piga moyo konde

Viuno vingi kama mwali wa kimakonde

Usipende hela kama mfuko

Au fanya unavyofanya upate zako

Vishawishi vingi binti sema na moyo wako

Na ujifunze pesa zinauza utu wako

Tajiri mtata kama Salah

Zipo ila sitoi me ni balaa

Unapenda hela zangu nami nazipenda pia

Kila mtu abaki na zake bye baby tutaongea

MWANAUME WA HIVYO WA NINI SASA!!!!! Ndiyo mnavyosema

Na ukiniomba kesho hunisikii tena

Kwani unauza nini dada

Hunitakii mema

Vanessa

Aje aje ajeeee me mtoto fulani ghali

Nihonge gari Ma sweet sweet baby

Wanna see you today unipeleke party

Aje aje ajeee njoo nikupe TBT

MWANA FA

Siyo kwa enzi ya Magufuli

Zali ilikuwa long siku hizi hakuna la mentali

Nikikuhonga na ukiniacha nitakujia usingizini

Naepusha shari matatizo yote ya nini

Hakuna kipya chini ya jua

Hata nisiyoyafanya nishayasikia

Ningekuwa mhongaji ningeshafulia wangu

Mademu wangu wa zamani wote wangekuwa maadui zangu

MWANAUME HOVYO WEWE!!!!! Ndiyo mnavyosema

Na ukiniomba kesho hunisikii tena

Kwani unauza nini dada

Hunitakii mema

Vanessa

Baki na hamu zako

Kiitikio

VANESSA

Baba bure huyuu!!!

Mwana FA

Hata pantoni lina staff

Vanessa

Unamwambia nani sasa! Unamwaaambia nani sasa!

Comments are closed.