The House of Favourite Newspapers

Mwili wa Baba Kanumba Waagwa Shinyanga, Kuzikwa Leo Simiyu

0
Mwili wa marehemu Charles Kanumba ukiwekwa eneo maalum kwa ajili ya kuagwa.

WANANCHI wa Shinyanga wamejitokeza kwa wingi kuuaga mwili wa baba mzazi wa aliyekuwa msaani wa Bongo Movies, marehemu Stephen Kanumba, mzee Charles Kanumba (71), kabla ya kusafirishwa kwenda katika Kijiji cha Nyakaboja, Busega mkoani Simiyu kumpumzisha kwenye makazi yake ya milele leo, Jumatano, Machi 11, 2020.

Ndugu wakiaga mwili wa marehemu.

 

Zoezi la kuuaga mwili huo  limefanyika jana Jumanne Machi 10, 2020, nyumbani kwake  Mtaa wa Magadula, Kata ya Ngokolo, Manispaa ya Shinyanga, huku ibada ya kumuaga ikiongozwa na mchungaji Benjamin Makaranga wa Kanisa la AICT Ngokolo.

 

Mke wa marehemu, Rehema Ramadhani,  akiaga mwili wa mumewe.

 

Akisoma historia ya marehemu kwa niaba ya familia,  Rubeni Zakayo, ambaye ni ndugu wa karibu na familia ya marehemu, alisema marehemu alizaliwa mwaka 1949 huko Busega mkoani Simiyu.

 

Mara baada ya kustaafu kazi serikalini mwaka 2015, alianza kusumbuliwa na maradhi ya nyonga, tumbo, magoti,  na kibofu cha mkojo, hadi umauti ulipomkuta Machi 8, mwaka huu.

 

Aliongeza kuwa marehemu ameacha mjane  na watoto saba, ambapo alifanikiwa kuzaa watoto tisa, lakini wawili wameshatangulia mbele za haki, watoto wa kiume watano na wa kike wanne.

 

 

Naye Mchungaji Zabroni Mang’wenghula kutoka Kanisa la AICT Ndala, aliwataka wananchi kumtumaini Mungu katika enzi za uhai wao, ili kujiweka tayari pindi watakapotwaliwa Naye.

 

Mchungaji Benjamini Makaranga wa kanisa la AICT Ngokolo akiongoza Ibada kumwaga marehemu  Charles Kanumba.

 

Mke wa marehemu, Rehema Ramadhani, mwenye nguo nyeupe akiomboleza msiba wa mme wake.

 

 

Ndugu wa karibu na familia ya marehemu, Rubeni Zakayo, akisoma historia ya marehemu.

 

Jeneza lenye mwili wa  Kanumba.

 

 

Leave A Reply