Mwili wa marehemu Gardner G Habash Wawasili Nyumbani Kwake Kijitonyama – (Video+Picha)
Mwili wa marehemu Captain Gardner G Habash leo Aprili 21, 2024 umewasili nyumbani kwake Kijitonyama ambapo utafanyiwa ibada maalum ya familia leo, na kesho kuagwa katika kanisa la KKKT Mbezi Beach saa mbili asubuhi na baadae viwanja vya Leaders Club.
Gardner G. Habash amefariki dunia alfajiri ya Aprili 20, 2024 katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) alikokuwa akipatiwa matibabu.