Mwinjilisti, Daudi Mashimo ‘Komando wa Yesu’ akiwaombea waandishi wa habari leo.
MWINJILISTI wa Kanisa la Calvary lililopo Mwenge jijini Dar es Salaam, Daudi Mashimo ’Komando wa Yesu’, leo amewaombea wanahabari juu ya utendaji wao kazi wa kila siku wa kuhabarisha umma jinsi matukio mbalimbali yanavyoendelea ndani na nje ya Tanzania.
Mwinjilisti huyo aliwaombea wanahabari katika Ukumbi wa Idara ya Habari (Maelezo).
Awali kabla ya kufanya maombi hayo, mwinjilishi tuyo alizungumzia juu ya utendaji kazi wa Rais wa Tanzania, Dk. John Pombe Magufuli kwa muda aliokaa tangu aingie madarakani.
Na Denis Mtima/Gpl.
Comments are closed.