The House of Favourite Newspapers

Mzee Majuto Arejea Kutoka India, Apelekwa Muhimbili – Video

MUIGIZAJI nguli nchini Tanzania, Amri Athuman maarufu kama Mzee Majuto amewasili nchini na kutua katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam akitokea nchini India alikokuwa amekwenda kwa ajili ya matibabu.

 

Mzee Majuto amewasili Airport leo Juni 22, 2018 majira saa 10 jioni na kupelekwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili ambapo atakua hapo kwa muda ili kukutana na wataalam kwa ajili ya uangalizi kukamilisha matibabu yake.

 

VIDEO: MZEE MAJUTO BAADA YA KUWASILI

Comments are closed.