The House of Favourite Newspapers

Mzee Mpili Atoa Tamko Zito

0

BAADA ya Yanga kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Simba, Jumamosi iliyopita, mwanachama maarufu wa Yanga, Mzee Mpili ameibuka na kutoa tamko zito.

 

Mzee Mpili ambaye kwa siku za karibuni amekuwa maarufu sana, amesema anachotaka kwa sasa ni fedha kiasi cha shilingi milioni moja alizoahidiwa na Ofisa Habari wa Simba, Haji Manara aliyesema angempatia endapo Yanga wataifunga Simba.

 

Akizungumzia ishu hiyo, Mzee Mpili alisema: “Simba wana maneno mengi hasa msemaji wao Haji Manara ambaye alisema kama tutawafunga atanipa fedha kiasi cha shilingi milioni moja.

 

“Hivyo namtaka Manara atimize ahadi yake, anipatie fedha zangu kwani mimi sikumuomba bali alitamka mwenyewe.

 

“Vijana walicheza mpira ambao sisi mashabiki tulikuwa tunautarajia, kuelekea mchezo wetu wa fainali ya Kombe la Shirikisho la Azam tunajiandaa kuhakikisha pia tunaibuka na ushindi na kuwa mabingwa.

 

Julai 25, mwaka huu, Yanga itapambana na Simba katika mchezo wa fainali ya Kombe la Shirikisho la Azam utakaochezwa Uwanja wa Lake Tanganyika, Kigoma.

 

Katika hatua nyingine, Mzee Mpili ameutaka uongozi wa Yanga kutolivuruga benchi la ufundi la timu hiyo linaloongozwa na Kocha Mkuu, Nasreddine Nabi kwani tayari ameanza kuisuka timu hiyo kuwa ya ushindani.

 

Msimu huu, Yanga imefundishwa na makocha wanne kwa nyakati tofauti ambao ni Zlatko Krmpotic, Cedric Kaze, Juma Mwambusi na Nsreddine Nabi.

 

HUSSEIN MSOLEKA

Leave A Reply