BAADA ya timu ya Kaizer Chief ya Afrika Kusini kutuma barua kwa uongozi wa Simba kuhitaji kumsajili mshambuliaji wao, Emmanuel Okwi raia wa Uganda, imebainika kuwa hatima ya mchezaji huyo kujiunga na timu hiyo ipo juu ya kocha mkuu Mbelgiji, Patrick Aussems.
Dirisha dogo la usajili la kimataifa linatarajiwa kufunguliwa mwezi Januari mwakani kwa mujibu wa Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa).
Akizungumza na Championi Ijumaa, Katibu wa Simba, Dr Arnold Kashembe alisema kuwa mezani kwake kuna barua nyingi lakini kuhusu Okwi kujiunga na timu ya Kaizer Chief ni mpaka kocha atoe maamuzi ya mwisho ndiyo wanaweza kumuachia.
“Mimi siwezi kuzungumzia hilo kwani kuna barua nyingi ambazo zinakuja lakini mwenye maamuzi ya mwisho ni mwalimu ambaye kama akiafiki sisi tupo tayari lakini pia kama ikitokea taarifa yoyote sisi tutawataarifu,” alisema Kashembe.
Comments are closed.