Mzungu Kichaa Amfagilia P Funk Kukuza Muziki Bongo – Video
MSANII wa Bongo mwenye asili ya Ulaya, Mzungu Kichaa, leo Jumanne 14, 2020, amempongeza prodyuza Paul Matthysse anayejulikana kwa jina la P Funk Majani kwa mchango wake mkubwa katika muziki wake (Mzungu) na kumfanya aeleweke katika jamii ya Tanzania kupitia ngoma yake ya ‘You Got Me’ na nyinginezo katika miaka zaidi ya kumi aliyokaa Tanzania.
Mzungu ameyasema hayo katika mahojiano na kipindi cha Bongo 255 kinachorushwa kupitia +255 Global Radio kila siku ya Jumatatu mpaka Ijumaa kwenye ofisi zake zilizoko kwenye jengo la Global Group Sinza-Mori jijini Dar.
Pia amewaomba wasanii wenzake kutokuwa wavivu kwenye kazi zao na wawe wabunifu kutoa kazi zilizo bora kukuza muziki wa Kitanzania.