MANABII wawili wa Kanisa la Repohim lililopo Sinza-Meeda jijini Dar es Salaam wamesimikwa rasmi kuwa manabii halali baada ya kupakwa mafuta ya upako kutoka kwa Askofu Dtk. John Mwakilema wa Kanisa la The Word of Prophecy Ministry lililopo mkoani Pwani ambapo watakuwa wakiwapa upako watumishi.
Askofu huyo akizungumza wakati wa hafla hiyo amewapongeza manabii hao kwa kufikia hatua hiyo rasmi na kuwataka kutenda vyema kwa watumishi wao katika kuwapa neno la kiroho na kuwapa mafuta ya upako.
Kwa upande wake Nabii Elisha na mkewe Olivia wameahidi kuwalisha watumishi wa Bwana Neno la Mungu ili watumishi hao waweze kurithi ufalme wa Bwana.
Aliongeza kuwa unyenyekevu ndiyo silaha pekee katika maisha ya mwanadamu na leo ndiyo sababu ameweza kupakwa upako kutoka kwa Askofu Mwakilema ili aweze kuwa nabii halali na watumishi wake waweze kulishwa vyema chakula cha kiroho.
Comments are closed.