The House of Favourite Newspapers

Namungo Yazitaka Pointi Tatu za Simba

0

HITIMANA Thiery, kocha mkuu wa timu ya Namungo amesema kuwa leo ataingia na mbinu mpya itakayompa nguvu ya kupata pointi tatu kwenye mchezo wao utakaochezwa Uwanja wa Taifa, saa 1:00 usiku.

 

Namungo iliyo nafasi ya tano kwenye msimamo ikiwa na pointi 28 baada ya kucheza mechi 16, itamenyana na Simba iliyo nafasi ya kwanza na pointi 41 baada ya kucheza mechi 16.

Akizungumza na Championi Jumatano, Thiery alisema kuwa moja ya mpango mkubwa wa timu yake ni kupata pointi tatu mbele ya Simba ili kuwajengea wachezaji wake hali ya kujiamini.

 

“Mchezo wetu utakuwa mgumu na wenye ushindani, unapocheza na bingwa lazima uwe na tahadhari kabla hajakuumiza, tunalitambua hilo na tutaingia uwanjani kwa tahadhari tukiwa na malengo ya kuzipata pointi tatu muhimu. Mashabiki watupe sapoti.”

Stori: Lunyamadzo mlyuka, Dar es Salaam

Leave A Reply