The House of Favourite Newspapers

Ndoa ya Tiko kufungwa katikati ya bahari

KILA mtu na staili yake! Ndivyo unavyoweza kusema baada ya msanii wa filamu na muziki, Tiko Hassan kusema kuwa ndoa yake itafungwa katikati ya bahari na itakuwa ni ya sapraizi.

Tiko aliiambia Shusha Pumzi kuwa tayari ana mchumba lakini hawezi kusema ndoa ni lini kwa kuwa anataka iwe sapraizi na itafungiwa ndani ya boti katikati ya bahari ili kuleta utofauti na ndoa za mastaa wengine.

“Ndoa yangu itakuwa ni ya sapraizi na itakuwa na utofauti kwani tutakodi boti na tutaenda kufunga ndani ya boti hiyo katikati ya bahari na sherehe itakuwa humohumo ili iwe ya aina yake ambayo kila mtu ataona kweli anayeolewa ni staa,” alisema Tiko

Stori: Mwadishi Wetu

Comments are closed.