TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imeitisha uchaguzi mdogo katika kata tatu, Nyahanga, Igumbilo na Kibosho Kati, zilizoshindwa kufanya uchaguzi Oktoba 28 kutokana na sababu mbalimbali. Kampeni zitaanza Novemba 17 hadi Desemba 7 na uchaguzi utafanyika Desemba 8, 2020.