The House of Favourite Newspapers

Wema Aanika Alivyoteseka Baada ya Zari Kupata Mimba ya Mondi

0

 

NDIO hivyo Bwana! Mrembo kutoka katika kiwanda cha filamu nchini Wema Sepetu hivi karibuni amesema kuwa hakuna kitu kilimuumiza baada yakuona Zari ametembea na aliyekuwa mpenzi wake Nasibu Abdul ‘Diamond’ kwa miezi miwili tu nakupata mimba.

 

Akizungumza na moja ya vyombo vya habari nchini mrembo huyo alisema kwamba hicho kipindi kilimuumiza sana na kumfanya kutambua kuwa kumbe yeye ndio alikuwa na matatizo ya uzazi na sio Mondi.

 

“ Zari alivyopata mimba ya Mondi nilikuwa na uhakika mimi ndio mwenye tatizo, iliniuma sana, nilikuwa nikimuangalia Zari kama vile anaishi yale maisha ambayo mimi ndio nimehangaika nayo, najiuliza nakosa nini?,” Alisema Wema

Leave A Reply