Jumapili ya Mei 13, 2018 ni siku ya kipekee kwa wapendanao wawili, Nevatusi Mango na Veronica Mkasa ambao walitimiza hatua muhimu katika maisha ya binadamu, pale walipofunga pingu za maisha katika Kanisa la St. Peters, Oysterbay jijini Dar es Salaam.
Ndugu, jamaa na marafiki walijitokeza kuwaunga mkono wawili hao katika shughuli hiyo muhimu, na kushuhudia wakivishana pete madhabahuni huku wakila kiapo cha kuishi pamoja mpaka kifo kitakapowatenganisha.
Global Publishers inawapongeza Nevatus na Veronika na tunawatakia maisha mema ya ndoa yenye furaha na baraka tele.
Comments are closed.