The House of Favourite Newspapers

Nguzo 5 Muhimu kwa Sokabet

0
Kikosi cha Majimaji.

JUZI Jumamosi mabingwa watete­zi wa Ligi Kuu Bara, Yanga, walikuwa wageni wa Majimaji, timu ambayo inad­haminiwa na Kam­puni ya Sokabet, timu hizo zilikutana kwenye Uwanja wa Majimaji, Songea la­kini kuna mambo kadhaa ya kujifunza.

Katika mchezo huo uliomalizika kwa sare ya bao 1-1, kuna mambo kadhaa ambayo yalionekana kuwa na maana kubwa katika soka la Ma­jimaji, Mkoa wa Ruvuma na Tanzania kwa jumla.

 

Mashabiki wakigombania jezi ya Majimaji.

1. FEDHA NI CHACHU YA MAFANIKIO

Hivi karibuni Majimaji ilikimbiwa na Kocha Kally Ongala kwa kile kili­chodaiwa kuwa ni kutokana na ku­tolipwa haki zake, hiyo ilisababisha hata morali ya wachezaji kushuka, lakini ujio wa Sokabet umeamsha moyo wa upambanaji wa wache­zaji na hata viongozi wenyewe wa­naonekana kuwa tayari kupambana kwa timu yao.

Mashabiki wa Yanga wakati timu yao ilipocheza na Majimaji juzi Songea.

2. SONGEA WANAPENDA MPIRA

Licha ya ukongwe wa Majimaji katika soka la Tanzania, lakini miaka ya hivi karibuni ilionekana kama tama­duni ya watu kuipenda timu yao ilipungua, lakini ujio wa Sokabet umeongeza chachu ya wadau kujitokeza kwa wingi kuisaidia na kuiunga mkono timu yao hiyo. Juzi wengi walijitokeza uwanjani na hata hamasa kabla na wakati wa mchezo ilikuwa kubwa.

Jerry Tegete akiwahamasisha mashabiki wa Majimaji kuishangilia timu yao.

3. WANAWAKE WA RUVUMA NI WANASOKA

Licha ya kuzoeleka kuwa soka ni mchezo unao­pendwa na wanaume lakini wa­nawake nao huwa wapo wenye mapenzi kama wanaume katika tasnia hiyo, upande wa Ruvu­ma kulikuwa na idadi kubwa ya mashabiki wa kike wasichana na wamama waliojitokeza uwanjani na baadhi yao walikuwa wame­vaa jezi za Majimaji mpya zilizo na nembo ya Sokabet, hiyo inath­ibitisha jinsi ambavyo wanawake wa Songea na Ruvuma kwa jumla walivyo tofauti.

Mechi ikiendelea.

4. TIMU ZA MIKOANI ZINAHITAJI WADHAMINI

Hali ya klabu za Simba, Yanga na Azam FC kupata wadhamini kila kukicha kumezifanya timu hizo kuwa na nguvu uwanjani na hata nje, lakini uwepo wa Soka­bet ndani ya Majimaji unathibi­tisha jinsi uwepo wa wadhamini unavyoweza kusaidia timu za mikoani kwa kuwa tangu kampu­ni hiyo ianze udhamini mwamko wa upambanaji ndani ya Majimaji umekuwa juu.

Jezi za majimaji zikichangamkiwa na mashabiki wa timu hiyo.

5. SOKABET INA NAFASI YA KUJITANUA

Kitendo cha Majimaji kuoneka­na kuwa na nguvu mkoani kwake kwa watu wake kuiunga mkono kwa kununia jezi zenye nembo ya mdhamini, kunamaanisha kam­puni hiyo ikiamua kutanua ud­hamini wake hata kwenye timu nyingine, inaweza kufanikiwa na itachangia ka­tika kukuza soka la ush­indani nchini, ili mwisho wake tupate wawakilisha imara wa ki­mataifa.

Akizungumzia juu ya mikakati yao, Mratibu wa Sokabet, Franco Ruhin­da, alisema: “Ni mapema kuelezea mikakati la­kini kadiri am­bavyo tunaen­delea kupata nguvu katika klabu tunayoid­hamini, hiyo itatupa nguvu ya kuongeza udhamini kwa Majimaji ama kwingine kwa kuwa kampuni yetu ina mikakati mikubwa na ina nia njema ya kukuza michezo ya Tanzania kwa kuwekeza, siyo ka­tika soka tu.

“Lakini ili kukamilisha hilo, nawaomba washiriki ambao wanaanzia umri wa miaka 18 kuendelea, kujiandikisha zaidi na kushiriki kubashiri matokeo katika tovuti yetu ya www.soka­bet.co.tz ambapo humo ndani mshiriki anaweza kushinda hadi shilingi milioni 100 kwa kubeti kwa buku tu.”

JOHN JOSEPH, Aliyekuwa Songea.

MANJI Amshitua Okwi, Atia Neno Kuhusu Bosi Wake Huyo

Leave A Reply