The House of Favourite Newspapers

Nisha Apokonywa Mabwana Zake Wawili, Aambulia Matusi

Nisha.

MSANII maarufu wa Bongo Movie ambaye huitendea vyema tasnia hiyo hasa akicheza scene za komedi, Nisha ameibuka na kueleza kusikitishwa kwake na kitendo cha kupokonywa mabwa zake wawili kwa nyakati tofauti kisha mhusika kumshushia mitusi hadharani.

Nisha kupitia ukurasa wake wa Instagram ameandika:

“Halafu me nimepooza kweli, nimechukuliwa wanaume mara mbili nikanyamaza kimya, hata kuna aliyeniibia akajifanya mbabe kuja kunichamba kwenye page yangu eti kama wa kwangu kwa nini sijatangazwa naye

“Nikamnyamazia hajui niling’atwa na nyoka sikutaka na yule anipe sumu ingine ningekufa kwa kipindi kile kuweka mahusiano nje ni mimi sikutaka, na nilijua hata yake yake yasingedumu.

“Natamani 😂yangejirudia sa hivi nichambane,nitupiane vidongo km Tanzania na Uganda 😂 KUMBE INAWEZEKANA EE 😐bad lucky wa sasa simwaniki maana ndo nishapiga nanga musije mbeba naye 😐,” ameandika Nisha.

Aidha Nisha hajabainisha ni mabwana wapi aliyopokonywa na alipokonywa na nani.

 

Comments are closed.