Nkomola Aanza Rasmi Mazoezi Yanga
MSHAMBULIAJI mpya wa Yanga, Yohana Nkomola, ameungana rasmi na wachezaji wa Yanga kwenye mazoezi yao baada ya kutoka katika majukumu ya timu ya taifa, Kilimanjaro Stars, ikiwa ni siku moja baada ya kutua nchini akitokea kwenye kikosi hicho.
Straika huyo ambaye tangu asajiliwe na Yanga hakuwahi kufanya mazoezi na kikosi hicho kutokana na kuwa kwenye majukumu ya timu ya taifa, leo kwa mara ya kwanza amefanya mazoezi ya pamoja na wenzake huku akikutana uso kwa uso na washambuliaji wenzake kama Amissi Tambwe na kiungo Papy.
Yanga imeendelea na mazoezi ya uwanjani leo Uwanja wa Uhuru jijini Dar kwa ajili ya maandalizi ya michuano ya FA na Ligi Kuu Bara inayotarajiwa kuendelea karibuni.
Na Musa Mateja/GPL
Comments are closed.