The House of Favourite Newspapers

Nusu Fainali Europa Moto Utawaka; Sevilla vs Man United leo

0

Vita ya Nusu Fainali ya Ligi ya Europa Kupamba Moto: Nani Ataingia Fainali – Ni Sevilla au Manchester United? Upande wa pili ni Inter Millan au Shaktar Donetsk?

 

Mtanange wa mechi za robo fainali za Ligi ya Europa umemalizika na sasa timu zinazoshiriki nusu fainali zimeshajulikana. Mechi wa kwanza ya nusu fainali ya Ligi ya Europa itafunguliwa pale ambapo Mhispania atakapochuana na Mwingereza, na mechi ya mwisho ni kati ya Muitaliano atakapomenyana na ‘Wana wa Ukraine’.

Mechi kati ya Wolves na Sevilla, Mhispania alionesha umwamba wake kama ‘old Spanish fox’ dhidi ya ‘fisi asiye na uzoefu kutoka Uingereza’.

Bayern Leverkusen walishindwa kutumia faida ya kutumia ardhi yao ya nyumbani na wakijikuta wakigaragazwa kwa goli 2-1 na Inter Millan.

Wakati ambapo Shakhtar Donetsk walitumia dakika 22 pekee kuwatoa vijana wa Marcel Koler – FC Basel kwa goli 4-1 na kufuzu hatua ya nusu fainali.

Wakati ambapo Jimenez alishindwa kutumia fursa ya penati kupachika bao, Ocampos alitumia fursa aliyoipata dakika 2 kabla ya mpira kumalizika akapeleka shangwe kwa mashabiki wa Sevilla na kufuzu nusu fainali.

Upande wa pili, Manchester United walitumia misuli yao kupambana na Copenhagen ambao waliweka ngumu mpaka kunako dakika ya 105 ambapo Bruno Fernandez alifunga goli kwa mkwaju wa penati na kumaliza mchezo kwa jumla ya goli 1-0.

Mchezo wa kwanza wa nusu fainali ya Ligi ya Europa utakutanisha Manchester United dhidi ya Sevilla, mchezo utakaochezwa siku ya Jumapili saa 4 usiku katika uwanja wa “Reinenergia” jijini Colgne – Ujerumani.

Ukweli ni kwamba, Sevilla hajawahi kufungwa na timu ya Uingereza kunako michuano ya Europa. Mpaka sasa amecheza na timu hizo mara 6 na kushinda mara 4 akitoa sare mara 2. Kwa upande wa mashindano, Sevilla akifuzu hatua ya fainali, itakuwa ni fainali yake ya 6 katika michuano hii.

Japokuwa, njia ya Sevilla haitokuwa rahisi kwani Manchester United pia wananafasi kubwa ya kushinda michuano hii sawa na Inter Millan. Nafasi ya Sevilla kushinda ni 31% wakati kwa Manchester United ni 38% na kama matokeo ya sare kwa mtanange huu ni 31%.

Mchezo wa pili ni kati ya Inter Millan na Shaktar Donetsk. Inter Millan anaonekana kuwa na nafasi nzuri ya kushinda mchezo huo japokuwa mchezaji wao Alexis Sanchez atakosekana kutokana na majeraha ya msuli wa paja. Endapo Inter Millan watafuzu hatua ya fainali, itakuwa ni nafasi kwa vijana wa Conte kubeba kombe la nne katika michuano hii ambayo walishakuwa mabingwa mara 3 (1990/91, 1993/94 na 1997/98).

Shaktar Donetsk nao sio timu ya kuibeza. Wamekuwa na msimu mzuri katika michuano ya Europa msimu huu pamoja na Ligi yao ya nyumbani. Hii itakuwa ni fursa ya Shaktar kubeba kombe la Europa baada ya miaka 11 ambapo mara ya mwisho walibeba kombe la ligi ya Europa mwaka 2008/09 walipowaburuza Werder Bremen kwenye fainali ya michuano hiyo.

Takwimu zinasemaje? Inter Millan ana 55% ya nafasi ya ushindi dhidi ya Shaktar, Shaktar ana 20% wakati nafasi ya kutoa sare ndani ya dakika 90 ni 25%.

Kwa upande wa odds, wataalamu wa Meridian wamempatia faida Muingereza. Ushindi kwa Manchester United unathaminiwa kwa odds ya 2.55, ushindi wa Sevilla umepatiwa odds ya 3.00 wakati matokeo ya sare ni 3.20. Ushindi wa Inter Millan umethaminiwa kwa odds ya 1.76, ushindi wa Shaktar umepatiwa odds ya 4.50 wakati matokeo ya sare ni 3.95.

Wataalamu wa Meridian wamekuwekea ofa ya machaguo zaidi ya 1,200 ambayo unawezakuyaangalia hapa.

Kuwa sehemu ya mchezo huu na ubashiri vile unavyopenda! Kwa odds nzuri, ofa kabambe za michezo na mambo kemkem, Meridian inakusaidia kuwa mshindi!

Jisajili na meridianbet hapa www.meridianbet.co.tz na furaha yako itaanzia hapo. Pakua App ya Meridianbet kwenye simu yako na uanze kubashiri kwa uhuru nyumbani kwako.

Pia unaweza kuwekapesa kwenye akaunti yako kupitia KwikPay, M-PESA au Airtel Money. Kumbuka, daima hauwezi kupoteza tiketi yako ya kwanza ukiwa na Meridianbet, tuna Bonasi ya 100% inakusubiri.

Meridian – Nyumba yenye odds bora na bonasi kubwa!

Leave A Reply