NYANGWINE AWAASA WAHITIMU KIDAO CHA SITA KUSOMA KWA BIDII
Mbunge wa zamani wa Tarime, Nyambari Nyangwine ambaye pia ni mwandishi wa vitabu vya riwaya leo amewaasa wanafunzi wanaohitimu kidato cha sita katika Shule ya Sekondari Kibaha, kusoma kwa bidii ili kufanikisha ndoto yao hapo baadaye.
” Ningewasihi sana wanafunzi hakuna silaha kubwa kama kujitahidi kwenye masomo ndio unaweza kupenya popote lakini bila elimu ni bure tu,na ni vyema mkatetema na masomo zaidi” alisema Nyambari ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye mahafali hayo.
Comments are closed.