Nyumba ya Wazanaki kivutio Viwanja vya Sabasaba jijini Dar
NA DENIS MTIMA/GPL
NYUMBA ya Kabila la Wazanaki imeonekana kuwa kivutio kikubwa katika maonesho ya Viwanja vya Sabasaba vya Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar kuliko vitu vingine baada ya kamera hii kunasa wananchi wakiingia kwa wingi kuishuhudia.
Mbali na nyumba hiyo, pia maonesho hayo yameonekana kupamba moto ikiwa leo ndiyo siku yenyewe ya Sikukuu ya Sabasaba baada ya wiki iliyopita kuzinduliwa na Rais wa Rwanda, Paul Kagame na mwenyeji wake, Rais wa Tanzania, John Magufuli. Hii ni mara ya 40 kufanyika kwa maonyesho hayo.