MAREKANI: Rais mteule wa Marekani, Donald Trump amesema kuwa ni ”heshima” kubwa kukutana na rais Barrack Obama katika mazungumzo ya mpito yaliofanyika katika ikulu ya White House.
Rais Obama amesema kuwa ametiwa moyo kuhusu mazungumzo yao ya maswala mbalimbali yaliochukua zaidi ya saa moja.
Trump ametilia shaka uraia wa rais Obama na kuapa kuharibu ufanisi wake wakati wa utawala wake.
Bw Trump kwenye kampeni alimweleza Bw Obama kama rais mbaya zaidi kuwahi kuongoza Marekani.
Wakati wa kampeni bwana Obama alisema kuwa bwana Trump ‘hafai’ kuongoza Marekani. Pia alisema Mwanarepublican huyo hana sifa na uwezo wa kuwa kiongozi wa Marekani.
Mfanyabiashara huyo tajiri kutoka New York, ambaye sasa ni rais mteule, kwa muda mrefu alitilia shaka uhalali wa habari kwamba Obama alizaliwa Hawaii, na alikejeliwa hadharani na Rais Obama.
Wawili hao walishauriana kwa zaidi ya saa moja afisi ya rais katika ikulu ya White House mnamo Alhamisi na walipojitokeza kwa wanahabari, walijaribu kuficha uadui kati yao.
Waliongea maneno mazuri kuhusu umoja na umuhimu wa kupokezana madaraka kwa amani.
Lakini picha zilizopigwa zinaonesha jambo tofauti, ukiangalia sura na mikono…
Hata hivyo Obama alisema kuwa ”anamuunga” mkono baada ya kumshinda Hillary Clinton.
Baada ya mkutano huo wa Ikulu rais Obama alisema kuwa kipaombele chake sasa katika miezi miwili ijayo ni kuhakikisha kuwa kundi litakalosimamia shughuli za mpito linafanikiwa kwa kiasi kikubwa.
Alisema kuwa wamezungumza sera za nyumbani pamoja na zile za kigeni na kwamba amefurahishwa na maoni ya Donald Trump kwamba yuko tayari kufanya kazi na rais Obama katika maswala yanayokabili Marekani.
Bwana Trump amesema kuwa yuko tayari kufanya kazi na rais Obama katika siku zijazo.
Comments are closed.