The House of Favourite Newspapers

OKWI: NIPO NJIANI NAENDA SAUZI KAMBINI KUJIUNGA NA SIMBA

0
Mshambuliaji Emmanuel Okwi raia wa Uganda.

Mshambuliaji Emmanuel Okwi raia wa Uganda, amethibitisha kuwa yupo njiani kuelekea nchini Afrika kusini kujiunga na wenzake wa Simba ambao wapo kambini.

Okwi ambaye amesajiliwa na Simba hivi karibuni, amethibitisha hilo kupitia ukurasa wake wa Instagram ambapo alikuwa akijirekodi ‘live’.

…Alikuwa live Instagram.

Wakati akiendelea na program yake ya kujirekodi ‘Insta Live’ huku akiulizwa maswali kadhaa na mashabiki wake mapema leo Ijumaa, alisema leo ataelekea Afrika Kusini kwa ajili ya kuanza mazoezi ya kujiandaa na msimu ujao wa 2017/18.

Simba ipo nchini humo kwa ajili ya maandalizi ya kujiandaa na msimu huo unaokuja.

Leave A Reply