The House of Favourite Newspapers

Ole Madeye Naye Autaka Uspika

0

Akiyewahi kuwa Mbunge wa Arumeru Magharibi, Goodluck Ole Medeye amechukua fomu kuwania kiti cha Uspika. Ole-Medeye aliyekuwa Mbunge na Naibu Waziri wa Kilimo kati ya mwaka 2010 hadi 2015 amechukua fomu hiyo leo Jumanne Januari 11, 2022 katika ofisi ndogo za CCM Lumumba jijini hapa.

 

Hatua hiyo inakuja baada ya aliyekuwa Spika wa Bunge hilo, Job Ngugai kujiuzulu Januari 6 mwaka huu. Ole Medeye ambaye anakuwa mtu wa pili leo kujitokeza katika ofisi hizo kuchukia fomu, akitanguliwa na Mbunge wa Geita, Joseph Musukuma ambaye pia amechukua fomu kuwania nafasi hiyo.

 

Hii ni mara ya pili kwa Ole Medeye kugombea nafasi hiyo kwani alishaahi kujitokeza tena mwaka 2015 akiwa Chadema, lakini hakufanikiwa.

 

“Kama mnavyojua dola ina mihimili mitatu ambayo ni Serikali, Mahakama na Bunge,kila kimoja kinatakiwa kufanya kazi kwa ufanisi,hivyo mimi kama nitakuwa Spika nitaweza kuimarisha mhimilili huo katika uongozi wangu,” amesema Ole-Medeye.

Leave A Reply