STORI: SAMSON JEREMIAH / GPL
MSANII wa Bongo Flava, Ommy Dimpoz mtunzi wa ngoma ya Kajiandae na mmiliki wa PKP Empire kwa sasa anamsimamia msanii Neddy Music, kafunguka mengi juu ya ubize wa wasanii wakubwa dhidi ya wasanii wanaochipukia kwa kutopokea simu za watu wa kawaida hususan za wasanii wachanga.
Dimpoz amesema alipata kazi kubwa hadi kukutana na msanii TID Mnyama pia alipata tabu kukutana na Ali Kiba kufanya naye ngoma ya pamoja.
Hayo aliyesema akiongea na East Africa Radio hivi karibuni katika kipindi cha Planet Bongo.
“Muda mwingine wasanii wakubwa tunapenda kujipa ubize usio wa maana, unapigiwa simu na kudai uko mikoani kumbe uko kitandani unachati na simu. Unakuwa huna nia ya kufanya kazi na msanii mdogo,” alisema Dimpoz.
Alipoulizwa kama aliwahi kutokewa na kadhia hiyo alisema ilimtokea wakati anataka kukutana na TID na Ali Kiba japokuwa ni watu poa sana na walimsaidia. Ila aliwataka wasanii chipukizi kujipanga wakati wanakwenda kukutana na wasanii maarufu ili waonyesha vipaji vyao.