The House of Favourite Newspapers

Omog Apewa Siku 10 Mapumziko

Omog.

UONGOZI wa Klabu ya Simba, umempa kocha mkuu wa timu hiyo, Joseph Omog siku zaidi ya siku kumi za mapumziko kabla ya kurejea kikosini kuendelea kuwanoa wachezaji wa timu hiyo wanaoendelea na mazoezi ya kujiandaa na michezo ijayo ya Ligi Kuu Bara.

 

Baada ya kuwa na mapumziko ya wiki moja, juzi Jumatatu Simba ilianza mazoezi kwenye Uwanja wa Chuo cha Polisi jijini Dar chini ya kocha msaidizi, Masoud Djuma raia wa Burundi.

 

Meneja wa Simba, Richard Robert, ameliambia Championi Jumatano, kuwa wanatarajia kuungana na Omog baada ya wiki moja na nusu ambazo ni zaidi ya siku kumi kwani likizo yake ni ndefu kuliko wengine.

 

“Vijana wanafanya mazoezi na kocha msaidizi wakati Omog akiwa mapumzikoni ambapo anatarajia kurejea kikosini baada ya wiki moja na nusu kuendelea kuwanoa vijana,” alisema Robert.

Omary Mdose, Dar es Salaam.

Comments are closed.