The House of Favourite Newspapers

Oyaa masela… yatima hadeki!

0

mpekeWanangu wa kitaani kwa fasi ya kijiweni inakuwa nini wazazi wenyewe? Si ni mpango mzima? Basi barida. Kama vepe sogea kwa saidi hii upate maudambwidambwi au mnabonga nene arifu? Basi mia! Welikamu kwa sana majembe yangu.

Wanangu nasikia kitu cha matumbo joto kwa wanene kwenye sekta nyeti kwa gavamenti kozi jamaa hakai kwa ofisi kama viongozi wengine. Ishu ni kuwashtukiza tu wana kuona kama mingo zinakwenda kimpango au magumashi?

Yaani machizi wangu nawishi mzazi jembe prezidaa aibuke kwa kitaa ya   bee aone masela hawana mbishe za kusaka mingo badala yake wanakula tu wepesi kwa striiti.

Bati wanangu kuna usemi kitaa kwamba hata kama huna mbishe ya kupiga siyo rizoni ya kuchili kitaa na kuanza kudandia ishu kwa fowadi ukisikilizia gavamenti ije ikuwekee mkwanja kwa poketi.

Masela tukumbuke kuwa yatima hadeki. Sasa wewe kama huna maparenti ndo kigezo cha kuanza kudeka? Kama una ndoto ni spidi yako tu kuamka na kuanza kuzikimbiza makachaa wangu. Ama nene? Basi mpango.

Ebana kwenye mastori yetu ya kitaa kuna mambo kibwena yanakrosi na ishu pekee ni kumiksi na kuchuja kuona kama zinafaa kwa walaji wangu?

Basi bana huku na huku nawaibukia machizi wangu kwa kitaa ya kati hapo kitu cha Nyamala kwa fasi ya Bongo tambarare. Ndani ya dakika bee pipo wanataka kujitoa kitu cha pumzi arifu.

Kuuliziza kwani vepe? Ndo nikapewa mchongo mzima kuwa hapo kwa kitaa kuna shori mmoko ni kisu au sumu ile mbaya aisee.

Unaambiwa mkidi mkare kiasi kwamba washkaji kitaa wanatafutana kinomanoma. Tangu manzi ametinga tauni siyo mtu wa kusebenza na wana. Unaambiwa mtoto ni mkavu mwanzo mwisho. Si unajua zile za uso wa mbuzi? Sema tu mbishe zake za kusaka bingo zinamfanya aweke tabasamu f’lani hivi fekelo ili apate wateja.

Yule mbebiz anadili na kusaplai kitu cha msosi kitaani. Heshima kubwa ipo kwenye chapati f’lani hivi anazomeki pale kitaa yaani zinavuta wanyama hadi wa ushuani. Kwani kuna tatizo? Hakuna tatizo ilimradi mkono uende kwa kinywa mazee.

Unaambiwa kasharobaro f’lani kakawekeza kiaje sasa? Unaambiwa mambo ya pamba nyepesi, taiti za hapa na pale, vitopu vya ukwehe na mavipodozi…sasa laifu linataka nini tena kwa mtoto wa kike? Ishu ni kukubalika mengine ni ektra tu kwenye hili laifu.

Huku na huku si msela mwingine akazama kwa shori? Hapo ndo vita ya dunia ilipoanzia aisee. Yaani chuma kwa chuma.

Mida f’lani hivi ya jioni chama langu wanarejea skani baada ya msoto wa dei nzima si ndo mtiti? Kuuliza vepe unaambiwa wana wanamgombea yule manzi aisee.

Mazee ilibidi watu wazima waingilie kati kutuliza mtiti wa maana na sasa laifu masti liendelee. Kama vipi ishu za kiloko tupa kule na kifuatacho ni kuzisanya mwanzo mwisho.

Mmenisoma masela? Kawikiendi ndo hakooo…sii yuu neksti wiki!

Leave A Reply