The House of Favourite Newspapers

P Diddy Atuhumiwa Kwa Ubakaji Katika Kesi Mpya

0
Rapa’ Mkongwe, Mtayarishaji Muziki na Mfanyabiashara, Sean Combs Diddy.

Rapa’ Mkongwe, Mtayarishaji Muziki na Mfanyabiashara, Sean Combs Diddy amefunguliwa mashtaka na Joi Dickerson-Neal ambaye amemtuhumu kumpa Dawa za Kulevya kisha kumdhalilisha Kingono, tukio lililotokea Januari 3, 1991

Mlalamikaji anadai baada ya kupewa Dawa na kudhalilishwa aligundua Diddy au PuffDaddy au P. Diddy alirekodi tukio hilo kwa siri na kuwaonesha watu kadhaa

Mwanasheria wa Diddy amedai tuhuma hizo ni za kutunga na mhusika ana nia ya kujipatia Fedha

Hivi karibuni Diddy pia alikabiliwa na tuhuma za aina hiyo kutoka kwa aliyekuwa mpenzi wake, nyota wa R&B, Casandra Ventura (Cassie) lakini walimaliza shauri lao nje ya Mahakama

Leave A Reply