The House of Favourite Newspapers

Pacman: Niko Fiti, Nitashusha Ndonga za Ukweli Dar Live

0

 

Nasibu Ra­madhan ‘Pac­man’

 

BAADA ya miaka sita kupita bila ya Ukumbi wa Dar Live uliopo Mbagala Zakhem, Dar kutumika katika mch­ezo wa Msamsumbwi, bondia Nasibu Ra­madhan ‘Pac­man’ atakuwa ni miongoni wa mwa mabondia watatu wa Tanzania wa­takaouwasha moto katika mapambano ya Kimataifa la kugombania ub­ingwa wa Global TV, Afrika Mashariki na Kati kwenye uku­mbi huo.

 

Video: Nasib Ramadhani Nitampiga vibaya Mzimbabwe Njooni Dar Live

Katika mapambano hayo yatayopigwa Ju­lai 22, mwaka huu kwenye ukumbi huo wa Dar Live na kurushwa mubashara na kituo cha Global TV Online kupitia tovuti ya www.glo­baltvtz.com, Pacman atacheza na Mzimba­bwe, Tinashe Mwadzi­wanaThe Chairman’ wakati Francis Miyey­usho ataonyeshana umwamba na Israel Kamwambwa raia wa Malawi huku Idd Pialali akitarajia kumalizana na Regin Champion kutoka DR Congo.

Tinashe Mwadziwana – ZIMBABWE

 

 

Pacman mwenye rekodi ya kuche­za mapambano 33, ameshinda 22, kati ya hayo 11 ni KO, amepoteza tisa, matatu ni KO huku akitoa sare mawili wakati mpinzani wake, The Chairman akiwa na rekodi ya kucheza mapam­bano 24, akishinda 12, sita kwa KO na amepigwa 12, moja kwa KO huku aki­toka sare moja.

Championi Ijumaa limefanya maho­jiano maalum na Pacman ambaye ana uwezo wa kurusha ngumi nyingi kwa mfululizo ‘cherehani’ kuelekea katika pambano hilo la kukata na shoka ambapo ameanza kufunguka alivyoweza kujiandaa:

“ Nimejiandaa vizuri na ko­cha wangu Christopher Mzazi ‘Mzazi Respect’ anani­simamia vizuri kwa sababu hili ni pambano la kimataifa, hivyo natakiwa kufanya vizuri.

“Hili si pambano la kwanza la kimataifa kucheza, nimeshacheza mengi nje ya nchi na ndani ya nchi, hivyo sina hofu hata kidogo.

“Naendelea kujifua vikali katika gym yetu ya No Talking Gym iliyopo Mabibo jijini Dar.

IDD PIALALI (TANZANIA)

 

UNAMZUNGUMZIAJE MPINZANI WAKO?

“Mpinzani wangu ni mzuri ila naamini mimi ni mzuri zaidi kuliko yeye, kwa jinsi nilivyojiandaa tuombe uzima hizi siku zilizobaki tuwe na afya njema na nguvu ili tuweze kufanya kazi tuliyotumwa na Watanzania.

 

USHAWAHI KUCHEZA PAMBANO LA UB­INGWA NDANI YA TANZANIA?

“Sijawahi, hili ni la kwanza kwangu, licha ya kuwa ni la kwanza la kugombania ub­ingwa, Watanzania wasiwe na wasiwasi.

IDD PIALALI (TANZANIA)

 

“Si kwangu tu hata kwa wenzangu wote tunaiwak­ilisha Tanzania tupo vizuri, wasituone wa kawaida, bali ni mabondia ambao ni wakali kwa hapa Tanzania na hao mabondia wanaokuja kutoka nje ya nchi wa­nakuja kupigwa tu na si kingine.

“Huko kwao wanaonekana wazuri lakini hapa kwetu ni wa kawaida tu kwa sababu tushaku­tana na mabondia wakali kushinda wao na tukawashinda.

 

MAPAMBANO YAKO YA NJE, NI LIPI LILIKUWA GUMU?

“Ni lile nililopigana mwaka jana dhidi ya bondia wa Uingereza, Thomas Ward. Huyu bondia alinisumbua sana japo nilimaliza

 mpaka mwisho pambano la raundi kumi, lakini nilipigwa. Pambano hilo lilifanyika Birmingham, Uingereza.

Chichi Mawe

 

ILIKUWAJE?

“Mpinzani wangu kila nilipokuwa napanga mikakati ya kumpiga nikawa nashindwa basi akawa ananipiga tu, unajua mpinzani wangu alikuwa yupo fasta sana yaani kabla sijapiga yeye tayari keshapiga, nilipigwa kihalali si­wezi kulalamika.

 

KWA NINI WANAKUITA PACMAN WA BONGO?

“Hilo jina wamenipa Watanzania kwa sababu wakati tunafundishwa na kocha wetu, tulikuwa tunaambiwa tufuate nyayo za yule Mfilipino, Manny Pacquiao ‘Pacman’ jinsi anavyocheza.

“Kwa kifupi Pacman ndiye aliyenifanya mpaka leo hii nimekuwa hapa, tulikuwa tukionyeshwa CD zake wakati anapigana, hivyo kocha akani­ambia anataka nicheze kama yeye, kuanzia hapo akaanza kunifundisha niweze kuwa kama Pac­man na Watanza­nia wenyewe ndiyo waka­nipa hilo jina mpaka leo naitwa Pacman wa Bongo.

 

KWA TAN­ZANIA, PAM­BANO LIPI LI­LIKUWA GUMU KWAKO?

“Ni moja ambalo nilicheza nikiwa na­chipukia , nilicheza dhidi ya Juma Fundi katika pamba­no la raundi 12. Wakati napam­bana naye, hapo ilikuwa ni baada ya awali kunipiga, kisha nikaomba tu­rudiane, akanipiga tena.

 

NINI SIRI YA MA­FANIKIO YAKO?

“Ukiwa na nidhamu kuanzia ndani ya ringi mpaka nje, moja kwa moja kiwango chako ki­nakuwa juu kwa sababu siku zote nidhamu matokeo yake ni mafanikio. Nime­fundishwa kuwa na nidhamu tangu naanza mchezo huu, kocha wangu amekuwa akini­sisitiza kila siku na nimekuwa ni­kifuata kile ninachoambiwa.

Israel Kamwamba – CONGO DR

 

UNAWAAMBIA NINI MASHABIKI WAKO?

“Nawasisitiza kuwa karibu na Global TV kush­uhudia mapambano haya kwani kupitia simu zao za mkononi, wanaweza kushuhudia live hata kama wakikosa fursa ya kufika ukumbini.

 

“Yaani Global TV imerahisisha mambo, mtu unaweza kukaa kwako ukaangalia kupitia simu yako, unaingia YouTube, unatafuta chaneli ya Global TV, basi unaangalia kila kitu moja kwa moja kutoka Dar Live. Mimi na wenzangu tu­tapambana kuhakikisha tunashinda katika ardhi ya nyumbani,” anasema Pacman.

Idd Pialali: Njooni Dar Live Mshuhudie Nitakavyomuua Mkongo

Katika hatua nyingine, pambano hilo la ngumi za kimataifa halitakuwa na kiingilio na mashabiki wataweza kulishuhudia mubashara (LIVE) kupi­tia simu zao za mkononi tu, kwani litaonyeshwa na Global TV pekee. Wadau na mashabiki wa­takaopata nafasi ya kuingia ukumbini wataingia kwa kadi maalum za mwaliko tu.

Regin Champion

 

Ili kulishuhudia pambano hilo kwa njia ya simu tena bure, hakikisha unajiunga (subscribe) na YouTube Chanel ya Global TV Online sasa hivi ili usipitwe. Ingia You Tube, tafuta GLOBAL TV ONLINE, kisha bonyeza neno subscribe pia bonyeza kikengele kidogo kilichopo pembeni yake ambacho kitakukumbusha kuangalia pambano hilo mara tu litaka­poanza.

 

Kama wewe umeshajiunga, basi hakiki­sha pia umebonyeza kikengele ili usipitwe na kila kinachoendelea Global TV. Pia un­aweza kutupata kupitia mtandao wetu wa www. globaltvtz.com. Usisubiri, jiunge sasa na Global TV ili uwe wa kwanza kuo­na ndondi za kimataifa.

JIUNGE SASA kwa kubonyeza HAPA: www.youtube.com/ user/uwazi.

IBRAHIM MUSSA | CHAMPIONI | Dar es Salaam

Leave A Reply