LICHA ya kufanya usajili wa zaidi ya wachezaji tisa wapya, Kocha Mkuu wa Singida United, Mholanzi, Hans van Der Pluijm, bado hajaridhishwa na usajili huo baada ya kuiambia kamati ya usajili ya timu hiyo kuwa anahitaji wachezaji wengine zaidi.
Mratibu wa kikosi hicho, Festo Sanga, ameliambia Championi Jumatatu kuwa Pluijm amewapa majina ya nyota kadhaa kwenye nafasi za kipa na kiungo kwa ajili ya kusajiliwa ili kukiimarisha kikosi chao.
“Tunaendelea na zoezi la usajili, kwani kocha katupa majina ya wachezaji anaowataka hasa kwenye nafasi za kipa na kiungo mmoja, ambapo mazungumzo na wachezaji hao yanaendelea na yakikamilika basi tutawaweka hadharani kama t u l i v y o fanya kwa wachezaji wote tuliowa s a j i l i , ” alisema.