Raila Odinga: Hatufanyi Maongezi Tena Na Ruto, Lazima Tumzuie Sasa
Kiongozi huyo wa Muungano wa Vyama vya Upinzani kupitia Azimio la Umoja One Kenya, Raila Odinga amesema wamefuta mazungumzo yote na Serikali baada ya Rais William Ruto kusaini Sheria ya Fedha
Amesema wanarejea katika kampeni za kuhamasisha migomo ya Wananchi dhidi ya jambo lolote la Serikali ikiwemo kutolipa Kodi zote ili kushinikiza Ruto aondoke Madarakani
Odinga ameongeza “Ruto anajaribu kuona kama tuna nia, nguvu na azimio la kupigana na udikteta. Tunapaswa kumzuia Ruto na tunapaswa kufanya hivyo sasa.”