Rais Magufuli Atembelea Meli Ya Hospitali Ya China
Rais John Magufuli leo ameitembelea na kuwaaga wanajeshi wa Meli ya Hospitali ya Jeshi la Maji la China ambayo imekuwa nchini kwa takriban juma zima ikitoa matibabu na uchunguzi kwa Watanzania kwa magonjwa mbalimbali. Meli hiyo ilikuwa imetia nanga katika bandari ya Dar es Salaam.