The House of Favourite Newspapers

Rais Magufuli Aagiza Ndege za Rais Zianze Kubeba Abiria – Video

Rais Dkt. Magufuli ameagiza kwamba ndege 2 kati ya ndege 3 za Rais, zipakwe rangi ya Air Tanzania na zianze kutumika kusafirisha abiria.

 

Ametoa agizo hilo leo Ijumaa Januari 11, 2019 wakati wa mapokezi ya ndege ya pili aina ya Airbus A220-300 iliyowasili katika Uwanja wa Ndege wa kimataifa Julius Nyerere (JNIA) jijini Dar es Salaam.

 

“Kwa kuwa rais mwenyewe hasafiri hovyo sasa zinakaa kufanya nini na moja ina uwezo wa kubeba watu 50. Hii haitabeba abiria pale tu ambako itakuwa inatumika,” amesema Rais Magufuliu.

 

Aidha Rais Magufuli ameshwashukuru wabunge wa Chama cha Mapinduzi kwa kuwezesha maendelo hayo kupitia kuunga kwao mkono bajeti inapopelekwa bungeni.

Airbus 220-300 imekuwa ni ndege ya 6 kuwasili nchini miongoni mwa 7 zilizonunuliwa na Serikali huku nyingine moja ikisubiriwa ambapo leo Rais amethibitisha kuwa ndege nyingine ya 8 inanunuliwa.

 

JIUNGE NA FAMILIA YA GLOBAL TV UPANDE MTANDAO WA MAFANIKIO

Bofya hapa kujiunga na familia ya Global TV Club ==> Global TV Family Club

Comments are closed.