The House of Favourite Newspapers

Rais Samia Afanya mazungumzo na Rais Yoweri Museveni na Rais Ruto, Tunguu Zanzibar

0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan akizungumza na wageni wake Rais Yoweri Museveni wa Uganda na Rais William Ruto wa Kenya walipowasili Ikulu ndogo Tunguu Zanzibar tarehe 14 Machi, 2024.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amefanya mazungumzo na Rais Yoweri Museveni wa Uganda na Rais William Ruto wa Kenya walipowasili Ikulu ndogo Tunguu Zanzibar tarehe 14 Machi, 2024.

Kwenye mazungumzo yao wamezungumzia masuala ya mtangamano wa Afrika Mashariki hususan umuhimu wa kuharakisha zoezi la kukusanya maoni ya Wananchi Juu ya muundo na maeneo ya kuangaliwa katika Rasimu ya Katiba ya Fungamano la kisiasa la Afrika Mashariki (EAC Political Confederation).

Zoezi hilo limeshafanyika katika nchi za Burundi, Uganda na Kenya na linatekelezwa na Timu ya Wataalamu inayoundwa na Wajumbe watatu kutoka kila nchi Mwanachama.

Rais Samia, Rais Yoweri Museveni wa Uganda na Rais William Ruto wa Kenya wakiangalia picha ya Viongozi wa Nchi mbalimbali za Afrika wakati Rais Museveni alipomkabidhi Rais Samia zawadi hiyo baada ya mazungumzo yao Ikulu ndogo Tunguu Zanzibar tarehe 14 Machi, 2024.

SIMBA na AL HILAL WAMTAKA DUBE BENCHIKH ATUA KAMBINI-KIVUMBI YANGA na AZAM MZIZIMA DERBY

Leave A Reply