Rais Samia Akutana Na Mtoto Hamimu Mwenye Matatizo Ya Ngozi, Ikulu Jijini Dar
Rais Samia Suluhu Hassan, leo April 26, 2023 amekutana na kuzungumza na mtoto Hamimu Mustapha Baranyikwa (15) ikulu jijini Dar es Salaam.
Mtoto Hamim mwenye matatizo ya ngozi ambaye ni mkazi wa Nyakanazi Mkoani Kagera amefika ikulu kwa ajili ya kumshukuru Rais Samia kwa msaada wa matibabu aliompatia katika Hospitali ya Taifa Muhimbili Jijini Dar es Salaam.
Rais alimuona mtoto huyo kwa mara ya kwanza wakati wa Ziara yake Nyakanazi Mkoani Kagera tarehe 16 Oktoba, 2022 na kuagiza apatiwe matibabu baada ya kuhangaika kwa muda mrefu.