Rais Samia Amteua Dkt. Saudin Jacob Mwakaje kuwa Mwenyekiti wa BASATA
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amemteua Dkt. Saudin Jacob Mwakaje kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA).
Dkt. Mwakaje ni Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Mjumbe wa Baraza lililomaliza muda wake.