Rais Samia Amteua Prof. Mark Mwandosya Kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi EWURA
Rais Samia Suluhu Hassan amemteua Prof. Mark Mwandosya kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji EWURA.
Prof. Mwandosya anachukua nafasi ya Prof. Jamidu Yahaya ambaye amemaliza muda wake.
Uteuzi huo umeanza Agost 15, 2022.