Rais Samia Atoa Pole Kwa Spika wa Bunge Kufuatia Kifo Cha Mbunge Irene Ndyamkama
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Samia Suluhu Hassan ametuma salamu za pole kwa Spika wa Bunge, Tulia Ackson Familia, Wabunge na Wananchi wa Mkoa wa Rukwa kufuatia kifo cha Mbunge wa Viti Maalum, Irene Ndyamkama aliyefariki dunia leo katika hospitali ya Tumbi Mkoani Pwani.