Yanga Princess Yapata Ushindi wa 1-0 Dhidi ya Simba Queens Katika Ligi Kuu ya Wanawake
Klabu ya Wanawake ya Yanga imepata ushindi wa 1-0 dhidi ya Simba Queens katika Ligi kuu ya Wanawake Tanzania.
Huu ni ushindi wa kwanza wa Yanga kwenye Ligi kuu ya wanawake tangu wapande daraja msimu wa 2019/20.
Yanga SC inafikisha alama 35 na kusalia katika nafasi ya 3 nyuma ya kinara Simba Queens (42) na Fountain Gates (35) iliyopo nafasi ya pili.