Rais Samia: Hakuna Mwenye Misuli Na Ubavu Wa Kuligawa Taifa -Video
Amesema “Nimesikia kuhusu Usalama, Amani, Umoja na Muendelezo wa Taifa letu, niliamua kunyamaza na ninaendelea kuwa kimya. Ninachotaka kuwahakikishia ni kuwa hakuna mwenye Misuli na Ubavu wa kuligawa wala kuuza Taifa hili.”
Rais Samia Suluhu Hassan ameyasema hayo katika Maadhimisho ya Miaka 60 ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) katika Chuo cha Tumaini Makumira Mkoani Arusha, Agosti 21, 2023
Aidha amesisitiza Serikali inawategemea Viongozi wa Kiroho katika kukuza na kusimamia maadili na Desturi za Nchi